July 21, 2015



Na Aidan Mlimila
Nakumbuka msimu uliopita siku ya mwisho wakati dirisha la usajili la majira ya kiangazi linafungwa mwandishi mmoja wa gazeti la Telegraph la Uingereza, Jim White aliandika "Ed Woodward is buying everything except what's needed" akimaanisha kuwa mtendaji mkuu wa Man Utd Ed woodward ananunua kila kitu isipokuwa kile ambacho kinahitajika.


Jim white aliandika maneno haya kwa sababu aliona Ed woodward ambaye ni mtendaji mkuu wa Man Utd alikuwa akisajili wachezaji kwenye nafasi nyingine za huku zile nafasi ambazo kweli zilikuwa zinamahitaji makubwa zikitelekezwa na hapo alikuwa akilenga nafasi ya ulinzi sana kwenye nafasi ya ulinz wa kati na sehemu ya kiungo cha ulinzi(defensive midfield).

Ni jambo ambalo liliweza kuonekana dhahiri wakati ligi ilipoanza Man Utd walionekana kuwa na mapungufu kwenye maeneo hayo although badae waliweza kukaa sawa na kumaliza ndani ya nafasi nne za juu.

Nikijaribu kuuangalia usajili ambao mpaka sasa ambao Man Utd wameufanya inaonekana ni kama Bw Ed woodward alimsikia Jim White wakati alipokuwa akikosoa usajili ambao Man Utd walikuwa wakiufanya.

Nasema hivi kwa sababu kwa usajili ambao mpaka sasa umefanyika nikiangalia na wachezaji waliopo naiona Man Utd mpya kabisa na nina amini itakuwa ni moja kati ya timu ambazo zitatoa changamoto kubwa sana kwenye harakati za kuwania ubingwa wa ligi kuu ya Uingereza na pengine wanaweza kurudia kwenye zama zile za Sir Alex Ferguson.Na bado Man Utd wanaonekana kuendelea na harakati za usajili kama ambavyo Louis Van Gaal alivyonukuliwa akisema kuwa bado wanaendelea na usajili.

Lakini pia kitu kingine ambacho kinanifanya niamini kuwa Manchester Utd wanaweza kurudia zama za Babu Fergie ni namna ambavyo Louis Van Gaal amekuwa akisimamia descipline za wachezaji wake ndani na nje ya uwanja kitu ambacho kilikuwa silaha kubwa sana ya Fergie katika kupata mafanikio yake. 

Katika timu zote ambazo Louis Van Gaal amepita kuanzia Barca,Bayern,Timu ya Taifa ya Uholanzi(The Orange) na nyinginezo Van Gaal amekuwa ni mtu ambaye amefanikiwa kusimamia nidhamu za wachezaji wake kitu ambacho kimemsaidia kurahisisha kazi yake kwa kiasi kikubwa.

Van Gaal amekuwa ni mtu ambaye hapendi mchezaji yeyote kuwa juu ya klabu isipokuwa yeye mwenyewe tabia ambazo zinafanana na zile za Fergie kitu ambacho kwa kiasi kikubwa kilimsaidia Sir Fergie kupata mafanikio makubwa akiwa na Man Utd ukiachilia mbali ubora wa mbinu ambazo alikuwa akizitumia.

Ni juzi hapa tumeona Van Gaal akimtema Victor Valdes kwa sababu aligoma kufanya mazoezi na timu ya kikosi cha pili kinachoundwa na vijana. 

Na LVG alinukuliwa akisema kwamba hawezi kumvumilia mchezaji yeyote ambaye haeshimu na haendani na falfasa za timu na ndiyo sababu akaamua kumtema Victor Valdes tukio ambalo nalifananisha na baadhi ya matukio ambayo Ferguson ameshawahi kuyafanya kipindi cha nyuma kwa kuwauza baadhi ya nyota wake ambao walishindwa kufuata kile ambacho yeye alikitaka na kuonyesha baadhi ya matendo ya utomvu wa nidhamu wachezaji hao ni kama David Beckham,Jaap Stam,Roy Keane,na Paul Ince.

Na hapo ndipo ambapo taratibu naanza kuiona Manchester Utd mpya na kurudia nyakati za Sir Alex Ferguson.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic