August 1, 2015


Rais wa Klabu ya Simba, Evans Aveva, leo Jumamosi anatarajiwa kuzindua rasmi Wiki ya Simba, ikiwa ni maandalizi ya kuelekea kwenye Tamasha la Simba Day, litakalofanyika Agosti 8, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.

Simba imeandaa tamasha hilo lenye lengo la kuwatambulisha wachezaji wake wote, kuelekea msimu mpya wa Ligi Kuu Bara.   

Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara, alisema katika wiki hii klabu yake itafanya mambo mbalimbali yakiwemo ya kijamii ili kujiweka karibu na mashabiki wake.

Aliyataja mambo ambayo yatafanyika katika wiki hii ni pamoja na uzinduzi wa maduka yatakayouza vifaa vya timu hiyo, uzinduzi wa matawi mapya, kutembelea wazee wa klabu hiyo, wadhamini wa klabu na kufanya usafi katika miji nchi nzima.

“Kesho (leo) rais atazindua rasmi Wiki ya Simba, kutakuwa na matukio mengi, katika wiki hii tutafanya mambo mengi ambayo yataifanya Simba kuwa klabu ya kipekee nchini.


“Katika wiki hii ya Simba, wachezaji watatembelea shule mbalimbali ili kuwapata wanachama wapya watoto wa Simba na katika Simba Day tunategemea mchezaji wetu mpya Laudit Mavugo atakuwepo,” alisema Manara. Simba inatarajiwa kucheza na FC Leopards ya Kenya katika siku yao.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic