August 1, 2015


Vital’O  ya Burundi inasisitiza haiwezi kumuachia straika wake Laudit Mavugo hadi ilipwe dau la usajili la dola 100,000 (Sh milioni 206), mchezaji huyo amesema hata kama dili lisipokamilika, hawezi kurudisha fedha aliyopewa na Simba.

Simba hivi karibuni iliingia mkataba na Mavugo ili aichezee timu yao lakini kumbe mchezaji huyo ana mkataba wa mwaka mmoja na klabu hiyo ya Burundi.

Sasa viongozi wa Vital’O baada ya kusuasua kwa muda mrefu katika kumruhusu Mavugo ajiunge na Simba, wamesema watafanya hivyo endapo klabu hiyo ya Tanzania itakubali kulipa dola 100,000 (Sh milioni 200) kuvunja mkataba.

Mavugo aliliambia Championi Jumamosi kutoka Burundi kuwa, Simba ilimlipa dola 10,000 (Sh milioni 20) ili asaini na ikamwambia itampa kiasi kingine kama hicho atakapotua nchini.

“Siwezi kurudisha fedha hizo kama dili langu hilo la kutua Simba litakwama kwani tayari nimeshazitumia kwa ajili ya mambo yangu ya kimaisha.

“Labda wakitaka wanisubiri hadi nitakapomaliza mkataba wangu na Vital’O mwakani nitakuja Tanzania kuichezea Simba,” alisema Mavugo ambaye ndiye mfungaji bora wa Ligi Kuu Burundi akiwa amefunga mabao 34.

 “Hata hivyo, binafsi napenda sana nije huko kuitumikia Simba, najitahidi kuwashawishi viongozi wangu ili waweze kumalizana nao. Simba wameniambia kuna kiongozi wao mmoja anakuja kumalizana na Vital’O ili mambo yaishe.”


Jana, Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara alisisitiza Mavugo atajiunga na Simba na kuichezea timu hiyo Jumamosi ijayo katika Simba Day dhidi ya AFC Leopards ya Kenya.

SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic