August 22, 2015


Kocha Mwingereza, Dylan Kerr amesema haoni sababu ya Simba kurejea katika kambi mjini Zanzibar.


Kerr amesema hayo baada ya uongozi wa Simba kutaka kikosi hicho kirejee kuweka kambi Zanzibar baada aya kocha huyo kukataa ile kambi nchini Oman.

Baada ya kufanya mazoezi kwa mara ya kwanza chini yake kwenye uwanja huo, Kerr raia wa Uingereza, amesema haoni haja ya kurudi tena Zanzibar kwani sehemu wanayotumia sasa kwa mazoezi ni nzuri.

 “Nilikuwa sijui kama kuna uwanja mzuri kama huu hapa Dar es Salaam, ndiyo maana nilitaka turudi Zanzibar baada ya safari yetu ya Oman kukwama lakini kwa sasa hakuna sababu yoyote ya kurudi huko,” alisema Kerr.


Simba itabidi ‘ijipige’ kidogo mfukoni kwani ili kuutumia uwanja huo inalazimika kulipa Sh 300,000 kila siku kwa ajili ya mazoezi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic