August 22, 2015



Wasanii Nasibu Abdul ‘Diamond’ na Ali Saleh Kiba ‘Aki Kiba’ kesho Jumapili wanatarajiwa kutumbuiza katika uzinduzi wa kampeni za mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli.

Diamond na Ali Kiba ni sehemu ya wasanii wengi wa muziki na wale wa filamu watakaotoa burudani kwenye uzinduzi huo unaotarajiwa kufanyika Viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam.

Kitendo cha Ali Kiba na Diamond kupanda jukwaa moja ni nadra kutokea kutokana na upinzani uliopo kati yao, hiyo watu watakaofika kwenye uzinduzi huo watapata burudani ya bure ya aina yake.

Mbali na kutamba na nyimbo nzuri kwa kila mmoja wao, kumekuwa na upinzani mkali kuhusu msanii mkali wa kutawala jukwaa, hivyo wawili hao wanatarajiwa kutoa burudani ya kiwango cha juu ili kuendelea kuthibitisha ubora wao.

Magufuli amepata nafasi hiyo baada ya kupita katika mchujo wa watangaza nia zaidi ya 40 waliojitokeza ndani ya CCM. Uchaguzi Mkuu unatarajiwa kufanyika Oktoba 25, mwaka huu.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic