August 19, 2015


Wakati uongozi wa Simba ukiendelea kujiandaa kuhusiana na mipango ya kuipeleka timu hiyo Oman kwenda kuweka kambi ya mwisho ya kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu Bara, mpango huo umepingwa vikali na Kocha Mkuu, Muingereza, Dylan Kerr.

Chanzo kikubwa cha Kerr kukataa mpango wa kambi hiyo ni kuhusiana na hali ya hewa ya huko ingawa amekiri kuwa anaweza kupata sehemu na viwanja vizuri kwa ajili ya kufanyia mazoezi.

Kerr amesema kwamba bado hajajua wapi wanaweza kwenda kuweka kambi kwa ajili ya maandalizi hayo lakini anaangalia pia uwezekano wa kurejea Lushoto, Tanga walikokwenda kuweka kambi ya awali kabla ya kutua Zanzibar.


Amefafanua kuwa, Oman kuna joto sana na hataweza kuwafua wachezaji wake ipasavyo na hiyo inaweza kuwasumbua kuelekea msimu ujao na kingine ni kwamba anahitaji kuwajenga zaidi kisoka wachezaji wake kuliko stamina katika wiki hizi chache zilizosalia kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu Bara, Septemba 12, hivyo sehemu ya joto kwa mbinu hizo haiwafai.

“Bado tunaangalia ni wapi pa kwenda kuweka kambi hii ya mwisho lakini Oman hapana, kule kuna joto sana, ni kweli kule kuna mazingira mazuri kwa ajili ya mazoezi lakini hali ya hewa ni tatizo. Nahitaji kuwapa zaidi mbinu za soka kwa sasa na si stamina kwa sana, hivyo Oman kule tutasumbuka.


“Tunaweza kuangalia kama ni kurejea Lushoto au kama tutapata sehemu nyingine nzuri zaidi kwa ajili ya mafunzo niliyokueleza basi tunaweza kwenda huko,” alisema Kerr ambaye ameiongoza Simba kwenye mechi saba za kirafiki hivi karibuni na kushinda zote kwa idadi ya mabao 18 ya kufunga na manne ya kufungwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic