August 4, 2015


Mshambuliaji mpya wa Yanga, Donald Ngoma amesema ana imani kubwa na kikosi chao cha Yanga.


Ngoma amesema presha kubwa aliyoipata kwenye michuano ya Kagame hasa baada ya kupata kadi nyekundu, imemfunza mengi kuhusiana na soka la Tanzania na ukanda wote wa Afrika Mashariki.

“Presha ililkuwa kubwa sana, niliona siku haziende. Lakini nimejifunza jambo na Yanga ina kikosi bora kabisa.

“Mimi nina imani kubwa na kikosi chetu kitafanya kazi nzuri tu kwa kuwa kuna ushirikiano mzuri, watu wanajituma na wanataka kushinda.

“Kama tulifanya makosa kwenye Kagame, basi tunaitumia nafasi hiyo kwa kuyarekebisha,” alisema Ngoma.


Ngoma raia wa Zimbabwe, alilambwa kadi nyekundu katika mechi ya kwanza tu ya michuano ya Kagame wakicheza dhidi ya Gor Mahia na Yanga ikalala kwa mabao 2-1.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic