August 22, 2015


Nyota wa Chelsea, kiungo John Obi Mikel, amemtibua Kocha wa Nigeria, Sunday Oliseh kwa kumuonyesha dharau na ameondolewa katika kikosi kitakachoivaa Taifa Stars mwezi ujao.

Septemba 5, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Taifa Stars itacheza na Nigeria ‘Super Eagles’ katika mchezo wa Kundi G kuwania kufuzu Kombe la Mataifa Afrika 2017.

Oliseh alisema amemuondoa kikosini Obi kutokana na kitendo chake cha kutowasiliana naye na hata alipofuatwa jijini London, England hakuonyesha kujali.

“Mwenzake Victor Moses wanayecheza naye Chelsea, nilipokwenda London nilikutana naye na akaniambia ana majeraha kidogo, huyu nilimuelewa. Lakini Obi nilimpigia simu hakupokea, nikamtumia ujumbe mfupi (SMS), hakujibu.


“Hatutaki kuonekana tunamtegemea mchezaji mmoja katika timu, kikosi kina wachezai 11 ambao wakishirikiana ndiyo timu inapata ushindi, siwezi kuzungumzia zaidi ya hapa,” alisema Oliseh ambaye ni nyota wa zamani wa Super Eagles.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic