August 3, 2015


Simba imeamua kuachana na mshambuliaji Laudit Mavugo.
Simba imefikia uamuzi huo baada ya kuona kuna hali ya sintofahamu iliyopitiliza.


Habari za uhakika kutoka ndani ya Simba, zimeeleza Mavugo ana mkataba na mmoja wa viongozi wa Vital’O ambaye amewasumbua kabla ya kufikia naye makubaliano.

“Lakini baada ya kumalizana na kiongozi huyo, viongozi walioingia madarakani nao wamekuja na mambo mapya.

“Sasa limekuwa jambo moja linazungumzwa kila wakati na haliishi, uongozi umeamua kuachana naye,” kilieleza chanzo.
Kutokakana na hali hiyo, Simba tayari imeanza juhudi za kupata mshambuliaji wa kati.


Hata hivyo, bado inaonekana kama mkongwe Mussa Mgosi na Hamis Kiiza wanaweza kuingoza safu hiyo ya ushambuliaji vizuri wakishirikiana na  vijana wengine kama Ibrahim Ajibu, Elius Maguri na wengine wanaochipukia.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic