October 26, 2015

BRAHIMI AKIPAMBANA NA OZIL NA KHEDIRA WA UJERUMANI

Beki kisiki wa Yanga na timu ya taifa, Taifa Stars, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, amekiri kukumbwa na ugumu wa kumkaba mshambuliaji wa Algeria, Yacine Brahimi, anayekipiga na timu ya FC Porto ya Ureno.



Stars na Algeria zinakutana Novemba 14 huku mechi ya marudiano ikichezwa Novemba 17 katika mchezo wa kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia zinazotarajiwa kufanyika Urusi mwaka 2018.

Algeria ndiyo timu bora Afrika kwa mujibu wa viwango vya Fifa na ndiyo timu iliyofanya vizuri zaidi kwenye Kombe la Dunia mwaka jana kwa upande wa timu za Afrika.

Cannavaro amesema mchezo huo utakuwa mgumu kwa upande wao kutokana na wachezaji wa timu hiyo kucheza soka la kulipwa Ulaya na kudai kuwa uwezo wa Yacine Brahimi ambaye ndiye anatarajia kumkaba ni mkubwa, hivyo anahitaji umakini wa hali ya juu.

“Inabidi tuombe Mungu atusaidie, Algeria ni timu namba moja Afrika, hivyo tunatarajia kukutana na ugumu wa hali ya juu, hasa ukizingatia wachezaji wao wengi wanacheza soka la kulipwa Ulaya.


“Brahimi ni mchezaji mzuri na ana uwezo mkubwa, hivyo nitakuwa na kibarua kigumu kuweza kukabiliana naye kutokana na uwezo alionao,” alisema Cannavaro.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic