October 26, 2015


Straika wa Yanga, Malimi Busungu,  ametakiwa kuongeza bidii mazoezi ikiwa ni pamoja na kugonga msosi wa kutosha kila siku ili aweze kurudisha stamina yake kama ilivyokuwa hapo awali wakati akijiunga na timu hiyo akitokea JKT Mgambo ya Tanga.


Busungu ambaye hivi karibuni amejihakikishia nafasi katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo kinachofundishwa na Mholanzi, Hans van Der Pluijm, ameanza kupoteza stamina, jambo ambalo linafanya awe anadondoka kila wakati uwanjani anapowania mpira.

Kutokana na hali hiyo, Pluijm kwa kushirikiana na daktari wa timu hiyo, Shecky Mngazija, wamemtaka Busungu kuhakikisha anajituma zaidi mazoezi ikiwa ni pamoja na kugonga msosi wa nguvu ili aweze kurejesha makali yake kama ilivyokuwa hapo awali.

Busungu alisema kuwa viongozi wake hao wamempatia ushauri huo hivi karibuni na tayari ameshaanza kulifanyia kazi.

“Hata kabla ya viongozi wangu kuniambia hivyo, hali hiyo nilikuwa tayari nimeshaiona, hata hivyo tayari nimeanza kuifanyia kazi na ninaamini baada ya muda mfupi nitakuwa fiti zaidi ya nilivyokuwa awali,” alisema Busungu.


Alipoulizwa ni kitu gani kimesababisha apoteze stamina yake ya awali, alisema: “Inawezekana ni majeraha niliyopata hivi karibuni lakini nitahakikisha narudisha makali yangu ndani ya kipindi kifupi.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic