October 26, 2015


Kufuatia hali ya kukosa mikwaju ya penalti iliyowakumba wachezaji wa Yanga, baadhi ya wachezaji wa timu hiyo, wametamka kuwa wanaweza wakaja kugomea kupiga mikwaju hiyo pale watakapopata katika michezo yake ya ligi kuu, kutokana na kuondokewa na kujiamini pale wanapoenda kuipiga.


Katika kipindi cha hivi karibuni kwenye michezo dhidi ya Toto na Azam, licha ya kikosi hicho kupata mikwaju hiyo, wachezaji wake Thabani Kamusoko na Donald Ngoma walijikuta wakiikosa na kuendeleza rekodi ya wachezaji wa kikosi hicho kukosa mikwaju hiyo.

Awali, Yanga ilikosa mikwaju mingi ya penalti kwenye mechi za Kombe la Kagame.

Mmoja wa wachezaji hao, Simon Msuva, alisema licha ya yeye kuchaguliwa kupiga mikwaju hiyo inapotokea uwanjani, kwa sasa anaweza asipige kutokana na kuondokewa na hali ya kujiamini pale anapokwenda kupiga, inayochangiwa na wachezaji wengi wa kikosi hicho kukosa mikwaju hiyo.

 “Unajua kuwa sasa yaani wachezaji tuna hofu kubwa ya kupiga penalti kutokana na hali hii ya kuikosa mikwaju hiyo pale inapojitokeza, jambo ambalo linatufanya kuendelea kuikosa mikwaju hiyo kama ilivyotokea kwa Ngoma leo (wiki iliyopita) tulipocheza na Toto.

“Lakini licha ya kuogopa mikwaju hiyo, naamini mwisho wa siku tunaweza kuja na jawabu la kupiga mikwaju hiyo, kwani kila kitu kina mwanzo na mwisho wake na naamini kocha tayari ameshaliona tatizo hili na atalifanyia marekebisho,” alisema Msuva mwenye mabao matatu katika ligi.


Kwa sasa mikwaju hiyo ya Yanga inapigwa na wachezaji, Haruna Niyonzima, Donald Ngoma pamoja na Msuva ikiwa ni baada ya kupewa jukumu hilo na kocha wa kikosi hicho, Mholanzi Hans van Der Pluijm.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic