Na Saleh
Ally
ELIUS
Mrugau Maguli ameifungia timu yake ya Stand United mabao matano, ikiwa inacheza
kwenye uwanja wake wa Kambarage ulio katika Kitongoji cha Majengo katika
Manispaa ya Shinyanga.
Maguli
amefunga bao moja wakati Stand United ikicheza nje ya Shinyanga. Alifunga bao
hilo katika mechi ya pili ya Stand United wakati ikicheza na JKT Ruvu kwenye
Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam.
Ukitaka
jumla, mshambuliaji huyo wa zamani wa Simba, amefikisha mabao sita na ndiye
anaongoza kwa ufungaji mbele ya wachezaji wa kigeni kutoka Yanga, Simba, Azam
FC.
Maguli
ambaye anaongoza kwa kufunga mabao mbele ya wachezaji wote wazalendo, amefunga
mabao manne katika kipindi cha kwanza kupitia dakika za 6, 19, 23 na 33. Mawili
amefunga katika kipindi cha pili ambayo ni dakika za 47 na 54.
Unaweza
kusema mgawanyo wa mabao yake kwa maana ya wakati gani, tayari ni mshambuliaji
anayeweza kufunga mabao katika kipindi cha kwanza, pia cha pili. Lakini anaweza
kufanya hivyo akiwa nyumbani au ugenini.
Bado
inaonyesha hivi; Maguli amefunga katika mechi nne kati ya saba ambazo Stand
United wamecheza nyumbani na ugenini.
Tena
inaonyesha hivi; Maguli amefunga mara mbili mabao mawili wakati Stand United
ilipoichapa African Sports kwa mabao 2-0 mjini Shinyanga, halafu akafanya hivyo
waliposhinda kwa mabao 3-0 dhidi ya Prisons ndani ya Kambarage.
Inaonyesha
hivi, mabao pekee ya Maguli yameisaidia Stand United kubeba pointi 12, wakati
yenyewe ina pointi 12 katika nafasi ya tano.
Mechi
dhidi ya African Sports walishinda 2-0, akafunga yote, wakashinda 1-0 dhidi ya
JKT, mfungaji pekee ni yeye, wakaitwanga Mbeya City 1-0, muuaji ni Maguli, juzi
wameilamba Prisons 3-0, ‘kaingia’ nyavuni mara mbili.
Pointi 12
zote za Stand United lazima umhusishe Maguli. Kwamba ndiye mhimili sasa wa
ushambulizi katika kikosi cha Stand United kinachofundishwa na Mfaransa,
Patrick Liewig.
Ukisoma
vizuri maelezo hayo, utagundua Maguli ni kati ya washambuliaji bora kabisa
ambao hata timu zetu kubwa zilikuwa zinawahitaji. Mfano zile zinazoshiriki
michuano ya kimataifa kama Yanga na Azam FC.
Wakongwe
wengine kama Simba ambao wanataka kurejea katika heshima yao, pia watakuwa
wanahitaji mtu kama Maguli.
Maguli ana
mabao sita, sawa ligi haijaisha, kweli ndiyo mbichi kabisa lakini ndiye
mshambulizi hatari zaidi kuliko wageni na wazalendo wote kwa kipindi hiki.
Hilo
halina ubishi, lakini hapohapo, huenda ndiyo wakati mzuri na mwafaka kujifunza.
Kwamba ndani ya kikosi cha Simba, unapozungumzia suala la usajili, Kamati ya
Usajili chini ya Zacharia Hans Poppe au ile ya ufundi pamoja na benchi la
ufundi, wana tatizo la kujua washambuliaji bora?
Unakumbuka
walimuondoa Amissi Tambwe, wakasema Kocha Patrick Phiri ndiyo amesema hivyo?
Yeye akasema hapana, hawezi kumuondoa mshambuliaji bora wa msimu uliopita.
Viongozi wakaendelea kusisitiza Phiri ‘amewaingiza chaka’.
Hilo
likapita, sasa limeiva suala la Maguli, ameondolewa Simba katika hali ya
kushangaza, imeshitua wengi kwa kuwa bado Simba haikuwa imekaa vizuri katika
safu ya ushambuliaji na ilihitaji mtu kama Maguli na tayari ilikuwa naye.
Maguli
kaondoka, Simba imemsajili mshambulizi ‘mtalii’, Pape N’daw, raia wa Senegal
ambaye hadi sasa ‘anauza sura’ tu. Taarifa zinaeleza huyo ndiye chaguo la Kocha
Dylan Kerr na mwingine aliyehusika kumshauri ni Collins Frisch mjumbe wa kamati
ya utendaji ambaye ni sehemu ya kamati hizo mbili. Sasa N’daw na Maguli ambaye
ni mzalendo, yupi ni msaada kwa Simba?
Baada ya
mechi sita, Simba imefunga mabao nane, kati ya hayo matano yamefungwa na Kiiza.
Utaona Maguli ana mabao sita, anazidiwa mawili tu na kikosi cha Simba lakini
hakuna mtu anayeweza kumfikia katika kikosi hicho.
Kamati ya
usajili na kamati ya ufundi, kweli wao kila wakati ni watu wa kuingizwa ‘chaka’
kama ilivyotokea kwa Phiri na sasa Kerr anayeendelea kupiga debe kwamba N’daw
atakuwa ni msaada kwa Simba!
Tujiulize,
kweli watu wa kamati hawana uwezo wa kufikiri, kuchanganua na kufanya uamuzi
sahihi na badala yake wataendelea kuingizwa chaka hivyohivyo na kuziachia timu
nyingine washambulizi bora wakati ligi inaendelea?
Kama
sivyo, basi kamati zenyewe zitakuwa na watu wasio makini ndani, huenda
wanaoamua kwa kufanya mambo kishabiki, kwa ubinafsi, ikiwezekana chuki au
hawajui mambo, ili mradi wanaungaunga tu!
Mafanikio
ya Maguli ni aibu nyingine kwa Simba, kamwe hawaikwepi na haina tofauti kubwa
na ile ya Tambwe ambaye aliondolewa akiwa mfungaji bora msimu mmoja kabla na
sasa ndiye mchezaji aliyefunga mabao mengi zaidi kama utajumlisha misimu miwili
ya 2013-14 aliokuwa mfungaji bora akitupia mabao 19 na ule wa 2014-15
aliopachika mabao 14.
Kuna kila
sababu sasa watu hao wa Simba waache ubishi, hata kama wanajua sana, basi
wajifunze kupitia makosa na si kuendelea wao kuwa makosa.
MECHI:
Stand 2-0 A. Sports Kambarage
Elius
Maguli 19
Elius
Maguli 33
JKT Ruvu 0-1 Stand Karume
Elius Maguli 6
Stand
1-0 Mbeya Kambarage
Elius
Maguli 47
Stand 3-0
Prisons Kambarage
Elius
Maguli 23
Elius
Maguli 54
WAFUNGAJI
WANAOONGOZA LIGI KUU BARA:
Elias Maguli Stand 6
Hamisi Kiiza Simba
5
Donald
Ngoma Yanga 5
Tambwe Yanga 4
Tchetche Azam 4
Atupele
Green Ndanda 3
Miraji
Athumani Toto 2
Fully
Maganga Mgambo 2
Busungu Yanga 2
Ali
Manzi Prisons 2
Jeremiah
Juma Prisons 2
Edward
Christopher Toto 2
0 COMMENTS:
Post a Comment