October 5, 2015


Kiungo Mshambuliaji wa Klabu ya Free State Stars ya Afrika Kusini, Mtanzania, Mrisho Ngassa, juzi Jumamosi aliisaidia timu yake kutinga hatua ya robo fainali ya Kombe la Telkom Knockout, baada ya kuichapa Bidvest Wits bao 1-0.

Katika mchezo huo uliopigwa katika Uwanja wa Goble Park jijini Bethlehem, Ngassa alifanikiwa kucheza kwa dakika zote 90.

Bao pekee la timu yao lilifungwa na kiungo wa timu hiyo, Danny Venter katika dakika ya 72 ya mchezo huo.

Ngassa alikuwa akihaha uwanja mzima na kuwapa wakati mgumu wapinzani wao huku akiwachosha mabeki waliokuwa wakitumia nguvu sana.

Baada ya mchezo huo, jana Jumapili Ngassa alitarajiwa kutua nchini kujiunga na kikosi cha timu ya taifa, Taifa Stars ambacho kinajiandaa na mchezo wa kusaka nafasi ya kufuzu Kombe la Dunia ambapo keshokutwa Jumatano kinatarajiwa kucheza dhidi ya Malawi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.


Ikumbukwe kuwa, uongozi wa Free State uliomba kiungo huyo achelewe kujiunga na kambi ya Stars iliyoanza Oktoba Mosi ili tu aweze kucheza mchezo huo ambao ulikuwa muhimu kwao.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic