October 7, 2015


 Na Saleh Ally
Leo ndiyo kile kipute kati ya Tanzania dhidi ya Malawi kuwania kucheza Kombe la Dunia.

Mechi hiyo inachezwa leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na inaonekana mashabiki wengi wana matumaini makubwa.

Ukubwa wa matumaini unafanya mechi hiyo ionekane kama ni lahisi jambo ambalo si sahihi.

Huenda wako wanaamini ni lahisi kwa kuwa Tanzania ilitoka sare na Nigeria ambao ni ulinganisho usio sahihi.

Lazima wachezaji Stars wacheze wakiamini mchezo ni mgumu na wanatakiwa kushinda leo ili kujiwekea mazingira bora hapo baadaye.

Malawi wana wachezaji nane wanaocheza nje ya nchi yao. Ni nchi za jirani za Msumbiji na Afrika Kusini ambazo zimepiga hatua kisoka zaidi yao.
Lakini wana timu ya wachezaji vijana zaidi. Hivyo lazima tukubali wana timu nzuri na yenye ushindani mkiubwa.

Ukichana na hivyo, wamekutana na Tanzania mara nne, wameshinda mara mbili, sare moja na tumewafunga mara moja. Lazima tukubali mechi ya leo ni ngumu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic