October 26, 2015


Uongozi wa Mbeya City upo katika hatua za mwisho za kukamilisha ripoti yao na kuipeleka kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutokana na kitendo alichofanyiwa kiungo wa timu hiyo, Joseph Mahundi na beki wa Simba, Mganda, Juuko Murshid cha kumpiga kiwiko na mwamuzi kutochukua hatua yoyote.


Kitendo hicho kilitokea katika mchezo wa Mbeya City na Simba uliopigwa kwenye Uwanja wa Sokoine, Oktoba 17, mwaka huu. Juuko alimpiga Mahundi  kiwiko wakati hana mpira na mwamuzi hakuchukua hatua yoyote.

Katibu wa timu hiyo, Emmanuel Kimbe, alisema kitendo kile kiliwasikitisha kama klabu, ndiyo maana wameamua kuchukua maamuzi ya kupeleka malalamiko sehemu husika.

Kimbe alisema kuwa katika mchezo ule ambao timu yake ilifungwa bao 1-0 lililofungwa na Juuko, kulikuwa na mambo mengi ambayo yalikuwa si ya kiungwana.

“Kitendo alichofanya beki wa Simba yule Mganda hakikuwa cha kiungwana kabisa na sisi tumeona hakuna hatua iliyochukuliwa na mwamuzi na wahusika wapo kimya, tulichoamua sisi ni kuandika barua ikiwa na vielelezo vyote pamoja na video ya tukio kwa TFF.


“Kwa sababu siku ile yalitokea matukio mengi  lakini yalikuwa yanafumbiwa macho, hivyo na sisi hilo hatulipi nafasi, maana Nyosso aliadhibiwa mapema, kwa nini wengine wacheleweshwe wakati matukio yapo wazi kabisa?” alilalama Kimbe.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic