October 9, 2015


Katika kuhakikisha safu yake ya ushambuliaji inafunga mabao mengi, Kocha Mkuu wa Simba, Dylan Kerr, ameanza kutengeneza mbinu mbalimbali zitakazowapa mabao mengi katika Ligi Kuu Bara.


Simba imefunga mabao saba katika mechi tano za ligi kuu msimu huu lakini bado kocha huyo amekuwa akiona safu yake ya ushambuliaji haina makali.

Katika mazoezi ya jana kwenye Uwanja wa Boko Veterani jijini Dar es Salaam yaliyoanza saa 3:00 asubuhi hadi 11:00 asubuhi, mbinu zilizotawala zilikuwa za kufunga.

Programu hiyo, iliwahusisha wachezaji wote wakiwemo mabeki, viungo na washambuliaji ambao ni Mussa Mgosi, Joseph Kimwaga, Pape Nd’aw na Danny Lyanga.

Awali aliwataka wachezaji kukimbia mbio fupi wakizunguka nusu uwanja, akahamia katika zoezi la kupiga pasi na kisha akaanza kutoa mbinu za kufunga.

Kerr aliwataka mabeki wa pembeni, Hassan Kessy, Emily Nimubona na viungo wa pembeni Simon Sserunkuma na Awadh Juma kuwapigia krosi wachezaji kwa ajili ya kufunga mabao.

Baadaye Kerr alianza kutoa mbinu za kufunga mabao nje ya mita 18 na mita 20 ambapo alikuwa akiwatumia viungo kuwatulizia mipira mirefu.


Baada ya mazoezi, Kerr alisema: “Nahitaji kuongeza makali ya kufunga, ndiyo maana naongeza mbinu kila siku.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic