November 28, 2015


Inaonekana beki raia wa Togo,Vincent Bossou amepania kuichukua nafasi ya nahodha wa Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro'


Kurejea kwa beki huyo, huenda kukawa kikwazo kwa mabeki wa kati wa timu hiyo, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Kelvin Yondani kwenye kikosi hicho kinachopigana kutetea ubingwa wa Ligi Kuu Bara.

Mtogo huyo, tangu atue Yanga amekuwa hapati nafasi ya uhakika ya kucheza katika kikosi cha kwanza kinachonolewa na Mholanzi, Hans van Der Pluijm.

Beki huyo, jana asubuhi alijitahidi kumshawishi Pluijm wakati Yanga ilipocheza mechi ya kirafiki dhidi ya Makongo Academy kwenye Uwanja wa Boko Veterani jijini Dar es Salaam.

Katika mechi hiyo, Yanga ilishinda mabao 3-0 yaliyofungwa na kipa Deogratius Munishi ‘Dida’ kwa penalti, Franky Gerald na Donald Ngoma, Bossou alicheza kwa kuelewana na Mbuyu Twite na kuzuia hatari langoni kwao.

Pluijm amesema kuwa kila siku anajaribu kombinesheni mpya ya wachezaji kwenye kikosi chake, na Bossou na Twite wamemfurahisha.


Pluijm alisema: “Nafurahia kuona mabadiliko ya Bossou kadiri siku zinavyokwenda kuanzia mazoezini hadi kwenye baadhi ya mechi anazocheza, hakuna mchezaji mwenye nafasi ya kudumu hapa, huyu akiendelea hivi atapata nafasi kikosini.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic