Na
Saleh Ally
WIKI
chache zilizopita, Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi
aliamua kutangaza kamati ya kuisaidia Taifa Stars ambayo ilikuwa inaongozwa na
Farouk Baghouza.
Lengo
lilikuwa ni kusaidia mchakato wa kwenda kupambana na Algeria kuwania kuingia
katika makundi kuwania kucheza Kombe la Dunia mwaka 2018 nchini Russia.
Mwenyekiti
wa kamati, Baghoza naye akaamua kuteua kamati ndogondogo kama vile, kama kamati
ya uhamasishaji na kadhalika.
Nilikuwa
sehemu ya kamati ya uhamasishaji nikiwa mwenyekiti na kazi yake kubwa ilikuwa
ni kuwahamasisha Watanzania kujitokeza kwa wingi uwanjani na kuishangilia timu
yetu ya taifa, Taifa Stars iliyokuwa inaanzia nyumbani.
Mara
tu baada ya kuingia kwenye kamati, ukaanza mzozo ambao ulitokana na mjumbe
aliyeteuliwa Shaffih Dauda kugoma uteuzi huo na badala yake akaendelea kuiponda
TFF na kamati.
Msisitizo
wake ulikuwa ni kwamba yeye hawezi kuingia kwa kuwa hakukuwa na njia ya mkato
ya kuisaidia Taifa Stars! Mzozo huo ulifika mbali kidogo alipoanza kuzozana na
Mahmoud Zubeiry na Maulid Kitenge ambao walifanya mahojiano kupitia kipindi cha
Sports Head Quarter cha EFM Radio. Hii ilikuwa ni siku moja tu baada ya mimi
kuwaomba waniache nikazungumze na Dauda kuhusiana na mambo mawili.
Moja
kuhusu kamati, kwamba kamati yetu si ya kiufundi au kuchangisha fedha. Badala
yake ilikuwa ni kuwahamasisha Watanzania kwenda uwanjani tu, hivyo haiusiani na
njia ya mkato hivyo aungane nasi na kama anaona hatafanya hilo jambo la
kiutaifa, basi akae kimya ili sisi tupigane, tukishindwa kuwashawishi watu,
kutakuwa na sehemu ya kujifunza.
Kitenge
na Zubeiry walishindwa kuvumilia baada ya kumsikia tena Dauda akiponda usiku
huo kwenye kipindi cha michezo cha Clouds. Mimi kidogo nilishituka, kwa kuwa
sikuona sababu ya Dauda kuiponda kamati wakati ule kwa kuwa sikumsikia
akizungumzia suala la kukuza vijana wakati wa mechi dhidi ya Nigeria au Malawi.
Vijana wanakuzwa pale Tanzania
inapokutana na Algeria tu? Au wote tuache timu ife peke yake halafu tuanze
kukuza vijana? Mbona hakusema kabla ya mechi hii!
Pia
nikawa najiuliza maswali, walioamini ndiyo wakati wa kukuza vijana kwa kuwa
tunakutana na Algeria. Wamewahi kujiuliza tuna viwanja vingapi vinatosha
kusaidia kukuza vijana? Sasa mbona hawakulilia ujenzi wa viwanja kwanza halafu
tufuatie kukuza vijana?
Hata
kama hakukuwa na kamati, bado angeweza kuzungumzia pia maana suala la vijana
pia haliwezi kufanywa na kamati ambacho huwa ni kitu cha muda mfupi kwa ajili
ya jambo fulani. Niliamua kuwa mchunguzi kwanza kwa kuwa wajumbe wa kamati
yangu waliokuwa kimya kabisa ni mimi na Edo Kumwembe.
Baadaye
niligundua kwa uchunguzi wangu, kwamba lengo lilikuwa ni kuanzisha mjadala
ambao ungesaidia mambo mengine kabisa ambayo hayakuwa na faida kwa taifa kwa
wakati huo. Wako waliniambia bila ya kamati, suala la kampeni kuita watu
lingekabidhiwa kwa Clouds FC ambayo ingeweza kuingiza mamilioni ya fedha, hivyo
haikumfurahisha Dauda, ndiyo maana akaamua kupambana. Sikuwaamini, kimyakimya,
nikasema “sidhani kama Shaffih anaweza kufanya hivyo”. Lakini nikaamua
kunyamaza, nikaendelea na uchunguzi wa taratibu ambao ulinifundisha mengi sana.
Nilijifunza
kupitia hilo suala la kamati, lakini bado safari hii nikajifunza mengi baada ya
kulazimisha kujilipia na kuongezewa kiasi cha fedha kwenda Afrika Kusini kwa
ajili ya kusaidia kuwaeleza Watanzania nini kilikuwa kikiendelea kwenye kambi
hiyo iliyokuwa jijini Johannesburg.
Moja,
nimegundua Watanzania wengi wanawatumia wanamichezo kwa kuwapumbaza wakianzisha
hoja kwa madai kwamba wanaipenda nchi, kumbe ni waongo na wazandiki wakubwa,
badala yake wanaangalia maslahi yao ndiyo maana utaona walifurahia sana Taifa
Stars kufungwa mabao 7-0, jambo ambalo ni usaliti wa wazi, ubinafsi wa hali ya
juu na uzandiki mkubwa usioweza kuvumilika.
Wako
wenye vita na TFF, walirudisha vita hiyo kwa Taifa Stars, walitaka ifeli ili
wathibitishe ubovu wa uongozi wa TFF, jambo ambalo pia naliita usaliti mkubwa
kwa nchi yetu. Ninaendelea kusisitiza kwamba wanafiki wamekuwa wengi kuliko
zamani, hofu yangu kwamba mchezo wa soka umebakiza asilimia 10 za kuweza
kuendelea kwa kuwa hata watetezi, nao wanaangalia maslahi yao badala ya maslahi
ya taifa.
Nimepigania
maisha ya mpira nchini kabla ya Leodeger
Tenga hajaingia madarakani. Rais wa TFF sasa, Malinzi amenikuta nikiendeleza
vita hiyo ambayo haitaisha hadi niondoke duniani. Na ikifikia ninamkosoa, kamwe
siwezi kukubali taifa langu kuanguka ili Malinzi aonekane amefeli. Akifanikiwa,
itakuwa furaha kwangu, akifeli nitamueleza ukweli lakini si chuki ya maisha
binafsi niingize na kuacha kuijali timu yangu ya taifa. Baadaye, nitaelezea kwa
nini nina hofu ya uraia ya baadhi ya watu kutokana na namna wanavyoweza kuibeza
Stars kwa kuwa tu hawakufaidika.
Lakini
pia niligundua kuwa kamati inapokuwa haina fedha, bado wengi hawawezi kuwa
watendaji. Wengi wangependa kila kitu kitangulize fedha mbele na suala la
uzalendo, linakuwa ni hadithi tu.
Watu
wengi walilazimika kutoa fedha zao za mifukoni, kama ambavyo Kamati ya Taifa
Stars ilivyolipia ndege na kutoa nusu ya fedha za kambi kule Afrika Kusini
ambayo ni mamilioni ya fedha.
Lakini
ilionekana kuna wengine wana uwezo wa kufaidika na imekuwa ni jambo la kawaida.
Baadaye nitakueleza kuhusiana na maofisa wa TFF ambao walifuja tu fedha na
hawakuwa na sababu ya kufanya hivyo wakati sisi tunasumbuka kwa kutoa fedha za
mifukoni kukamilisha mambo yaende sawa hasa katika uhamasishaji.
Kingine
ambacho niligundua, kwamba wachezaji wa Taifa Stars wengi wao ni vijana na si
wazee kama wengi wanavyoamini au kupiga kelele, eti tunataka vijana. Wastani wa
umri wa kikosi ni miaka 23 na wakongwe hawazidi watano.
Lakini
ni kikosi chenye wachezaji wengi wasiojitambua, wasioelewa nini nchi yao inataka
au wananchi wanataka kuona nchi yao inafika wapi ikiwezekana wanaona Yanga,
Simba na Azam FC ni kubwa kuliko timu ya taifa!
Niligundua
wachezaji wengi wa Taifa Stars, bado hawajajua umuhimu wa kikosi hicho na
ukubwa wake kwa hisia za ndani ya mioyo yao na sikutoka kwenye ubongo wao.
Huenda kwa kuwa wamepita njia ya mkato kufika hapo, au wameingia kwa ulaini
kutokana na ushindani kuwa duni, hivyo kila kitu kinakuwa lahisi kabisa kwao.
Nitakuelezea
namna nilivyolazimika kuzuia ndege ya Fastjet tena kwa ugomvi mkubwa kwa dani
35 isiondoke kwenye Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Oliver Tambo jijini
Johannesburg kwa kuwa wachezaji watano walichelewa kuingia ndani ya ndege tena
kwa sababu za kipuuzi kabisa.
Achana
na hiyo, nitakueleza namna wachezaji wa Stars walivyoshindwa kupumzika usiku
kwa kulala mapema, badala yake wakaonyesha tabia za ajabu, za ‘uswahilini’
kwetu, hali iliyonipa hofu na kuanza kaumini safari yetu bado ni ndefu sana.
MAKALA
haya, mwanzo yalianza kutoka katika gazeti la Championi. MUEDELEZO, SOMA SEHEMU
YA PILI.
0 COMMENTS:
Post a Comment