Na
Saleh Ally
UTAONA
katika sehemu ya kwanza na kuelezea mambo mengi ambayo niliyaona baada ya
kuingia kwenye kamati ya Saidia Taifa Stars ishinde.
Nilikuwa
Mwenyekiti wa kamati ndogo ya uhamasishaji. Kazi yake kubwa ilikuwa ni
kuhamasisha watu kwa wingi kwenda Uwanja wa Taifa kuishangilia Taifa Stars
ikipambana na timu ngumu na kigogo wa Afrika ambaye anajulikana duniani kote.
Jana
nilieleza nitazungumzia mambo mengi, nikianzia hali ilivyokuwa katika kamati,
wale waliojitoa katika kamati akiwemo Shaffih Dauda na kuanza kushambulia, uozo
wa ndani ya TFF lakini nidhamu mbovu na aina ya wachezaji tulionao.
Kelele za kamati:
Hii
ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuingia katika kamati yoyote ile. Nilikubali
baadaya kuchaguliwa na Mwenyekiti Farouk Baghoza, sikuona shida kwa ni suala la
utaifa. Kuita watu kwa wingi kuishangilia Taifa Stars zaidi ililenga kuipa
nguvu timu.
Inawezekana
kabisa, TFF wangeweza kufurahia mapato zaidi. Lakini sikuwa na mgawo au
motisha, badala yake niliangalia suala la kuunganisha Watanzania kwenda
kuishangilia timu kwa nguvu zote.
Dauda
aligoma kuingia kwenye kamati, kama nilivyooleza jana ikafikia Maulid Kitenge
na Mahmoud Zubeiry kuamua kujibu mashambulizi kutokana na kuchoka kwa kuwa
Dauda aliendelea kushambulia akidai kamati haina lolote. Kilichowauma wawili
hao, kamati tuliyokuwepo haikuwa ya ufundi au kuchangisha fedha. Badala yake
kuwahamasisha Watanzania waende kwa wingi uwanjani ikiwezekana kuwazomea sana
Waalgeria na kuipa nguvu Taifa Stars.
Kwa
kuwa nilikuwa mwenyekiti wa kamati, nilipinga Kitenge na Zubeiry kumshambulia
Dauda kama alivyokuwa akifanya. Niliwashauri sisi tuonyeshe ni wakongwe kuliko
yeye ambayo ni hali halisi. Nikawashauri tuangalie tunachotakiwa kufanya katika
kamati yetu hiyo ndogo na si kulumbana.
Baada
ya hapo sikuridhika, nilitaka kujua kipi hasa kinamfanya Dauda aanze kuhubiri
kuhusu suala la vijana leo! Taifa Stars ina mechi siku 14 zijazo, halafu eti
mtu anaanza kuhubiri ukuzaji wa vijana. Nilianza kuona kama miujiza, sikukubali
kwamba alikuwa na nia nzuri ya kuitetea nchi, nilipata harufu ya maslahi
binafsi, nikaamua kuingia ndani zaidi kutaka kujua.
Uchunguzi
wangu uligundua mambo mengi sana, nitaanza na machache. Baadhi ya niliopita
nikichunguza walinieleza haya. Moja, Clouds FM wamekuwa wakiingia mikataba ya
kuzitangaza Taifa Stars, safari hii kwa kuwa kulikuwa na kamati ambayo ilikuwa
ikiwashawishi watu wengi kujitolea kutangaza bure, hilo lilimuudhi Dauda kwa
kuwa kimaslahi, anakuwa hafaidiki. Maana kuna suala la kamisheni kwake!
Sikuamini
kwa kuwa namjua Dauda ni mzalendo. Lakini nikajiuliza, katika mechi ambazo
Clouds FM ilifanya kazi ya kuitangaza mechi hiyo, mbona Dauda hakuzungumzia
suala la vijana?
Nikajiuliza
tena, hivi Dauda alitaka vijana wa Tanzania wakue ndani ya wiki mbili ili
waichezee Taifa Stars dhidi ya Algeria? Maswali yakawa mengi, lakini kimyakimya
nikasema; “Shaffih ni mtu mwema, hawezi kufanya mambo ya kipuuzi kama hayo.”
Tofauti
nilifikiri Dauda angeweza kuamini kuona taifa letu lilikuwa vitani. Hadithi ya
Algeria ni timu kubwa na ngumu kufungika, si jipya. Huenda limezungumzwa miaka
nenda rudi na hata watoto wa shule ya msingi wanalijua. Vipi ndani ya wiki
mbili kabla ya Stars kuivaa Algeria ndiyo iwe ishu kubwa?
Kama
taifa linakwenda vitani, halafu raia mwema anawavunja nguvu wanajeshi wake,
unaweza kuamini mtu huyu ana mapenzi na taifa lake? Nikajijibu kimyakimya: “Shaffih
ni mtu mwelewa sana, huenda alighafirika tu, baadaye ataelewa.”
Nilijua
kamati isingecheza, isingeshangilia lakini ilikuwa ikijitahidi kufanya kila
linawezekana kupitia timu hiyo inayoonekana si nzuri kwa wengine ijaribu.
Lakini imeshindikana.
Ajabu
zaidi, kweli katika maendeleo ya soka sasa unaweza kuzungumza kamati na
kuifanya mjadala badala ya kusema Taifa Stars inapaswa iungwe mkono vipi? Hivi
ukisikia Mtanzania mwenzako anasema anafurahia kuona timu ya taifa imefungwa,
unaweza vipi kupima uwezo wa ufikiri, uzalendo wake na moyo wa utaifa?
Niliamua
kuachana na hayo, najua ni ya kupita na huenda nashauri wanaozungumzia ukuzwaji
wa vijana, bora wakaangalia zaidi na kulipigania suala la viwanja bora ili
tuwasaidie vijana.
Kikubwa
niwapongeze kila walioacha kazi zao na kupambana kuhakikisha Taifa Stars
inakuwa ina nguvu. Imefungwa 7-0, nimefungwa mimi, wewe na mzalendo yoyote,
achana na wanaoamini kipato kinazidi utaifa.
Kamati
yetu haikuwa na fedha, tulijichangisha kupitia bajeti tuliyojiwekea, hatukuifikia
badala yake tukapita tukiwaomba watu watusaidie matangazo, stori, makala
ilimradi kuwahamaisha tu Watanzania. Ahsante sana Waandishi, wahariri na
viongozi wakuu wa vyombo vya habari mliojitolea, bila ya kuangalia maslahi
kwanza.
Nikiachana
na hilo, sasa naingia katika mambo kadhaa niliyoyaona ndani ya siku zaidi ya 10
nilizokuwa katika kamati.
Maofisa
wengi wa TFF si watu wanaolenga kutaka kuendeleza mpira. Wengi ni wazandiki,
waliolenga kujifaidisha, wanaotaka kushibisha matumbo yao na kamwe hawana nia
ya kusaidia Taifa Stars kama watu wengi ambavyo wamekuwa wakifikiria.
Nitakueleza kwa nini.
ENDELEA
KUSOMA SEHEMU YA TATU.







0 COMMENTS:
Post a Comment