November 11, 2015


 
 Na Saleh Ally, Johannesburg
Hisia zisizo sahihi, au hisia za kizamani ni sehemu ya mambo ambayo yamekuwa yakiiangusha michezo nchini.


Mchezo wa soka, ndiyo unaathirika sana na wakati mwingine wanawake huonekana kama adui.

Lakini nchi zinazopiga hatua kimichezo ukiwemo wa soka zinakwenda njia tofauti kabisa na Afrika Kusini.

Angalia mwandalala huyo mrembo ambaye ndiyo kiungozi wa mazoezi ya viungo ya timu ya vijana ya taifa ya Afrika Kusini.


Vijaan chini ya miaka 23, wengi wao wakiwa wanacheza katika timu za Ligi Kuu na zile za ligi daraja la kwanza. Maana yake wana fedha na wanalipwa mishahara mikubwa, unaweza kusema wana maisha yao mazuri.

Lakini mazoezi yao ya viungo yanaongozwa na dasa mrembo kabisa ambaye kama ingekuwa Tanzania, angeonekana ni adui.
 

Mfano, timu ingepoteza mchezo, gumzo lingekuwa huyo dada. Lakini kama timu ingecheza vibaya, dada angekuwa gumzo.

Bado unaweza kujiuliza pia, wachezaji nao wangeweza kuwa na nidhamu kama wanayoonyesha hao wa Afrika Kusini? Wangefanya kazi yao bila ya kuangalia suala la urembo wa huyo dada?

Timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 23 ndiyo imekuwa kipenzi cha Wasauzi na wakati mwingine wanataka ile ya wkaubwa ivunjwe na hii ya vijana ipewe jukumu la wakubwa.

Chini ya Kocha Owen Da Gama na msaidizi wake, Shaun Bartlett imekuwa ikiendelea kung’ara.

Jiulize hili kuhusu nchi yetu. Kweli tunakwenda sawa? Kulalamika ndiyo imekuwa dira katika kila jambo, inatusaidia?





0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic