November 11, 2015


Kocha Msaidizi wa timu ya vijana ya Afrika Kusini chini ya miaka 23, Shaun Bartlett amesema kikosi cha Tanzania, Taifa Stars kina uwezo wa kuitoa Algeria lakini haitakuwa lahisi.


Kikosi cha Barltett ambacho Kocha Mkuu ni Owen Da Gama kiliifunga Stars kwa mabao 2-0 katika mechi mazoezi ya kirafiki iliyopigwa kwenye Uwanja wa Eldorado jijini Johanneburg, jana.

Bartlett amesema Algeria ni timu bora na yenye wachezaji wazoefu, lakini katika soka mambo hubadilishwa na wanaojiamini na kujituma.


“Utulivu linakuwa ni jambo namba moja, lazima kile ambacho wachezaji wameagizwa na mwalimu na wanajua ni kipi cha kufanya basi kifanyike kwa uhakika.

“Kwanza kabisa lazima wachezaji wajiamini kuwa wana kazi kubwa kubwa na inawezekana. Wakiingia uwanjani wanaamini haiwezekani, ndiyo itakuwa hivyo,” alisema Bartlett aliyewahi kuichezea Charton Athletics iiliyokuwa inashiriki Ligi Kuu England.

Mshambuliaji huyo wa zamani wa Bafanabafana amesema mabadili katika mchezo wa soka ni timu ndogo kuifunga timu kubwa.

“Kama timu kubwa zitaendelea kufanya vizuri dhidi ya timu ndogo, maana yake hakuna mabadiliko. Matokeo yasiyotarajiwa ndiyo mabadiliko. Yakitokea ndiyo yanaongeza radha ya soka na lazima yafanywe na wanaojiamini kuwa inawezekana.”


Stars inaivaa Algeria Jumamosi jijini Dar es Salaam, katika mechi inayotarajiwa kuwa kali na ya kusisimua.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic