November 14, 2015


Kiungo mwenye kasi wa Free State Stars ya Afrika Kusini, Mrisho Ngassa, amempongeza Mbwana Samatta kutwaa tuzo ya ufungaji bora Afrika, kwani yeye alijaribu kuitwaa akashindwa.


Ngassa wakati huo akiichezea Yanga mwaka jana, alifikisha mabao sita katika michuano hiyo akilingana na El Hedi Belameiri wa ES Setif, Haythem Jouini (Esperance) na Ndombe Mubele wa AS Vita.

Kwa kuwa hakushiriki mchezo wa fainali, Ngassa alikosa tuzo hiyo ya mfungaji bora japokuwa jina lake limo kwenye orodha ya wafungaji bora msimu huo wa 2014.

Ngassa amesema: “Nilijaribu kuwa mfungaji bora mwaka jana, lakini mambo yakashindikana ila mwenzangu Samatta ameweza, hongera kwake.”

Wikiendi iliyopita, Samatta akiichezea TP Mazembe, alifunga bao moja na kufikisha mabao saba huku akitengeneza lingine na kuiwezesha timu yake kushinda mabao 2-0 dhidi ya USM Alger katika mechi ya fainali ya marudiano jijini Lubumbashi, DR Congo.

Mazembe ilitwaa ubingwa huo wa Ligi ya Mabingwa Afrika huku Samatta akipewa tuzo ya ufungaji bora.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic