November 13, 2015


Huku pazia la usajili wa dirisha dogo Tanzania Bara likitarajiwa kufunguliwa Jumapili ya wiki hii, uongozi wa Klabu ya Yanga umetamka kuwa hautafanya usajili wowote ule mpaka uhakikishe unawauza baadhi ya wachezaji wake.


Yanga ambayo ilianza mazoezi wiki hii baada ya mapumziko ya muda, inashika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi ikiwa na pointi 23, mbili nyuma ya vinara Azam FC.

Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro, amesema wamepania kufanya hivyo kwa kufuata ripoti ya kocha wa kikosi hicho aliyopendekeza kutosajiliwa mchezaji yeyote mpaka pale watakapohakikisha wanauza baadhi ya wachezaji.

“Licha ya dirisha dogo la usajili ndiyo linataka kufunguliwa lakini kwa upande wetu bado hatuna mawazo ya kusajili wachezaji wengine kutokana na hawa waliopo kocha kupendekeza kuendelea nao wote katika michezo ijayo.

“Pale tutakapohitaji kufanya usajili ni lazima tuhakikishe tunawauza wachezaji waliopo ambao wanatakiwa na timu nyingine kwa ajili ya kukusanya fedha za kununua wachezaji bora zaidi ya watakaokuwa wanaondoka ndani ya timu yetu,” alisema Muro.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic