November 11, 2015

HALL (KULIA) AKIWA NA KOCHA WA YANGA, HANS VAN DER PLUIJM.

Kocha mkuu wa timu ya Azam, Muingereza Stewart Hall ametoa onyo kali kwa timu zote za ligi ambazo zitakutana na kikosi chake zijipanga kikamilifu kuweza kuwazuia kwani amepanga kutoa dozi kwa kila timu.

Azam chini ya Stewart imefanikiwa kuwa kileleni mwa ligi ikiwa na pointi 25 ikifuatiwa na Yanga yenye 23, ambapo katika mchezo ujao wa ligi kuu Desemba 12, mwaka huu kikosi hicho kitashuka dimbani kumenyana na Simba katika mchezo utakaopigwa Uwanja wa Taifa, Dar.

Stewart amesema kuwa kwa sasa hawataangalia aina ya timu wanayokumbana nayo uwanjani kwani lengo lao ni kuhakikisha wanachukua pointi tatu za wapinzani wao hao kwa ajili ya kuzidi kujikita katika kilele cha msimamo wa ligi.

“Kwa sasa hatutaangalia aina ya timu ambayo tunakutana nayo katika michezo yetu ijayo kwani sisi lengo letu ni moja tu kuhakikisha tunashinda ili kuweza kuendelea kujiwekea pengo kati yetu na Yanga ambao wapo nyuma yetu kwa ukaribu.


“Nina uhakika wa kufanya hivyo wa kushinda kila mchezo wetu kwani kikosi chetu kinaundwa na wachezaji wenye viwango lakini pia wenye kutaka kushinda katika mechi zetu hivyo haitakuwa shida sana kupata pointi tatu kwenye mechi zetu,”alisema Stewart.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic