November 30, 2015


Kikosi cha Kilimanjaro Stars kimeng’olewa katika michuano ya Chalenji baada ya kufungwa katika mechi ya robo fainali kwa mikwaju ya penalti 4-3.


Stars ndiyo ilikuwa ya kwanza kufunga bao kupitia nahodha wake, John Bocco lakini wenyeji wakasawazisha kwa mkwaju wa penalti baada ya Shomari kapombe kumuangusha mshambuliaji wao.

Katika mikwaju ya penalti, Kili Stars ilipoteza penalti kupitia kwa Jonas Mkude kabla ya Shomari Kapombe naye kupoteza zote zikipanguliwa na kipa wa Ethiopia.

Kili Stars ilikuwa na nafasi zaidi ya kushinda baada ya kpata nafasi nyingi zaidi za kufunga ikiwemo ile ya Said Ndemla aliyeshindwa kuitumia akiwa amebaki na lango tu.

Kili Stars inayonolewa na Abdallah Kibadeni ilishambulia mara 15 katika kipindi cha kwanza huku wenyeji Ethiopia wakishambulia mara 6 tu.

Suala la kupoteza nafasi, limechangia kuiondoa Stars katika michuano hiyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic