November 27, 2015

WAWA

Siku chache baada ya kiungo mshambuliaji Brian Majwega, raia wa Uganda, kutua Simba, amefunguka kuwa amepania kuonyesha uwezo wa juu huku akijinadi kuwa ameshamwaga siri za kumzima beki kisiki wa Azam FC, Paschal Wawa.


Majwega amejiunga na Simba hivi karibuni ambapo awali alikuwa akiitumikia Azam, usajili wake umekuwa gumzo hasa kwa kuwa Azam bado imesema kuwa ina mkataba naye.

Wakati hayo yakiendelea, Majwega ameliambia Championi Ijumaa kuwa, amepanga kuonyesha kiwango kikubwa kama akipewa nafasi katika mechi ijayo ya Ligi Kuu Bara ambayo itazikutanisha timu hizo mbili mnamo Desemba 12, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
 
MAJEGWA
“Naamini TFF (Shirikisho la Soka Tanzania) itanipa haki yangu kwa kuwa mimi ndiyo nipo sahihi tofauti na Azam, pia siyo kwamba nitaihofia Azam tutakapokutana, nikipewa nafasi nitafanya makubwa na kuhakikisha naisaidia Simba kushinda siku hiyo.

“Kuhusu Wawa najua cha kufanya kwa beki kama huyo ambaye anawadhibiti halafu anapanda kuja kushambulia. Kwanza ni kuwazonga langoni mwao muda wote ili asipate nafasi ya kujipanga lakini vitu vingine nitaongea na wachezaji wenzangu na tutajua nini cha kufanya,” alisema Majwega.


SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic