April 18, 2016

WASHINDI HAO PAMOJA NA OFISA WA AZAM TV ALIYEOONGOZANA NAO, IRADA WAKIWA NDANI YA LA CORUNA NA MWENYEJI WAO AITWAYE MARIA...

Washindi wa “Kwea Pipa Kwenda Spain na Azam Sports HD”, wametua katika mji wa La Coruna ambao ni makao makuu ya klabu ya Derpotivo la Coruna inayoshiriki la Liga.

Washindi Ismail Salim na Jamal Mussa wametua mjini la Coruna baada ya safari ya zaidi ya saa 24 wakipita katika miji ya Zurich, Uswiss na Madrid, Hispania katika ya kufika hapa la Coruna.

Washindi hao watajumuona kuangalia moja kwa moja mechi ya La Liga kati ya Derpotivo ambao watawakaribisha Barcelona kwenye Uwanja wao wa Riazor wa mjini hapa.

Angalia baadhi za picha wakiwa jijini Madrid kuja hapa na baada ya kufika hapa ambako wamefikia katika hoteli ya kisasa kabisa ya Melia.

HAPA WAKIWA MADRID KABLA YA KUONDOKA KWENDA LA CORUNA



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic