July 26, 2016


Kocha Mkuu timu ya Mpira Tanzania ‘Taifa Stars’, Charles Boniface Mkwasa ameita kikosi cha wachezaji 24 watakaoanza kambi ya awali kuajindaa na mchezo dhidi ya Nigeria utakaofanyika Lagos, Septemba 2, 2016.

Kwa mujibu wa Mkwasa, timu hiyo itaingia kambini Agosti 1, 2016 na itadumu kwa siku tano tu kabla ya kuvunjwa na kuitwa tena mwishoni mwa mwezi Agosti, 2016 kujiandaa na kambi ya mwisho na moja kwa moja itakuwa ni kwa ajili ya safari kwenda Nigeria.

Katika kikosi hicho, Mkwasa hajaita nyota wa kimataifa akiwamo Nahodha, Mbwana Samatta wa FC Genk ya Ubelgiji na Thomas Ulimwengu wa TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kwa sababu ya majukumu waliyonayo kwenye klabu zao kwa sasa.

Kadhalika, nyota hao wataungana na wenzao nchini Nigeria kwa kuwa mchezo huo upo kwenye kalenda ya CAF na ni wa mashindano. Mchezo huO ambao ni wa kukamilisha ratiba, Mkwasa amesema utakuwa mgumu kwani Nigeria wamebadili benchi la ufundi hivyo kila timu inaungalia mchezo huu kwa jicho la pekee.

Wachezaji walioitwa ni:
Makipa:
Deogratius Munishi
Aishi Manula
Benny Kakolanya

Mebeki:
Kelvin Yondani
Aggrey Morris
Oscar Joshua
Mohamed Husein ‘Tshabalala’
Juma Abdul
Erasto Nyoni

Viungo:
Himid Mao
Mohamed Ibrahim
Shiza Kichuya
Jonas Mkude
Ibrahim Jeba
Mwinyi Kazimoto
Farid Mussa
Juma Mahadhi
Hassan Kabunda

Washambuliaji:
Simon Msuva
Joseph Mahundi
Jamal Mnyate
Ibrahim Ajib
John Bocco
Jeremia Juma


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic