August 20, 2016

Wakati dunia ikiamini kuwa kiungo Marouane Fellaini atakuwa mmoja wa wachezaji ambao wataondoka klabuni hapo mara baada ya kutua kwa Kocha Jose Mourinho hali imekuwa tofauti kabisa na vile ambavyo ilikuwa ikitegemewa.

Fellaini ambaye ameanza katika mechi zote za ushindani chini ya kocha huyo alionyesha kiwango kizuri katika mchezo wa timu yake hiyo dhidi ya Southampton, juzi na kuwashangaza wengi waliojua kuwa safari yake imewadia.   






 Akizungumzia juu ya kufanya vizuri kwa mchezaji huyo ndani ya muda mfupi licha ya wengi kumuona ameshindwa maisha ndani ya klabu hiyo maarufu kwa jina la Mashetani Wekundu, Mouringo alifafanua kuwa yawezekana yote hayo yalianza kutokana na simu.

“Naweza kusema kuwa labda simu ilichangia kwa kuwa mara baada ya kiutambulishwa tu kuwa nimekuwa kocha wa United nilimpigia simu.

“Nadhani hata yeye hakutegemea kwa kuwa alijihisi ni mchezaji ambaye hapendwi hapa, lakini yawezekana simu ilirejesha kujiamini kwake na ndiyo maana nacheza vizuri sasa,” alisema Mourinho.

Fellain, kiungo wa zamani wa Everton ambaye alishindwa kuwa na maisha mazuri klabuni hapo kuanzia kwa kocha David Moyes ambaye ndiye aliyemsajili na hata kwa Louis van Gaal ambaye alitimuliwa msimu uliopita.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic