August 20, 2016

Klabu ya Crystal Palace imethibitisha kumsajili mshambuliaji Christian Benteke kutoka Liverpool kwa ada ya pauni milioni 32 ambayo ni kubwa kuwahi kutokea kwa klabu hiyo kusajili.
   



Benteke alikuwa jijini London tangu jana Ijumaa kwa ajili ya vipimo vya afya ambapo baada ya kukamilisha taratibu alitambulishwa rassmi.


Usajili huo umekuja baada ya mchezaji huyo kutokuwa katika wakati mzuri kwa kushindwa kutamba Liverpool tangu alipotua akitokea Aston Villa.

Akizungumzia juu ya usajii huo, Benteke ambaye ana umri wa miaka 25 alisema: “Nina furaha kutua hapa Crystal Palace, nategemea kufanya mengi kwa kujituma.”

Benteke amefunga mabao mabao 51 katika Premier League katika misimu minne aliyocheza katika ligi hiyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic