August 21, 2016

Rais mstaafu wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete ameongoza mamia ya wananchi kuuaga mwili wa mwanamuziki mkongwe wa taarabu Shakila Said Hamis maarufu kwa jina la ‘Bi Shakila’, leo jijini Dar.

 
Bi Shakila enzi za uhai wake.

Mwili wa Bi Shakila Said umehifadhiwa katika nyumba yake ya milele maeneo ya nyumbani kwake Mbagala Charambe jijini Dar.


Rais Mstaafu awamu ya nne, Dkt Jakaya Kikwete (wa tatu kulia) akijalidiliana jambo na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,  Nape Nnauye (pili kushoto).

Makamu wa Rais Mh, Samia Suluhu akijadiliana jambo na mmoja wa waombolezaji nyumbani kwa marehemu, kabla ya maziko kufanyika. Bi Shakila, amefariki ghafla nyumbani kwake, huko Mbagala Charambe.

 Rais Mstaafu Dkt Jakaya Kikwete akizungumza na waombolezaji.

Katibu MKuu wa Shirikisho la Wanamuziki Tanzania, John Kitime akiweka saini kitabu cha maombolezo cha Bi Shakila Said, nyumbani kwa marehemu Mbagala Charambe jijini Dar.

Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan akiweka saini kitabu cha maombolezo cha Bi Shakila Mbagala Charambe jijini Dar, kushoto ni  Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye.

 Baadhi ya wanamuziki wakongwe na Bongo Fleva wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kushiriki mazishi ya Bi Shakila huko nyumbani kwake Mbagala Charambe jijini Dar.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye akiwa na baadhi ya waombolezaji wengine wakiwemo wasanii wa muziki wa kizazi kipya, Banana Zorro na wanamuziki wakongwe wakiwa kwenye mazishi ya Bi Shakila, huko nyumbani kwake Mbagala Charambe jijini Dar.

APUMZIKE KWA AMANI, AMINA!

PICHA: MICHUZI-MATUKIO

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic