August 29, 2016


Nyota wa zamani wa Arsenal, Thierry Henry  ameanza rasmi kazi ya Kocha Msaidizi wa Ubelgiji.

Henry ametua jijini Brussels na kwenda moja kwa moja kwenye hoteli ya timu hiyo ambako alijitambulisha mwenyewe.

Baada ya hapo, alianza kazi akiwa chini ya Kocha Mkuu, Roberto Martinez, ambaye ni kocha wa zamani wa Everton.

Henry ambaye alianza kwa kuwa kocha wa vijana wa Arsenal kabla ya kuamua kufanya kazi ya uchambuzi, inaonekana sasa ameamua kuwa siriaz na kazi ya ukocha.

Kikosi hicho chenye mastaa kibao, kinajiandaa katika mechi dhidi ya Cyprus.

KIKOSI KAMILI CHA UBELGIJI:
MAKIPA: Courtois, Mignolet, Sels 
WALINZI: Alderweireld, Kabasele, Lombaerts, J. Lukaku, Meunier, Vermaelen, Vertonghen
VIUNGO: De Bruyne, Defour, Dembele, Fellaini, Nainggolan, Witsel
WASHAMBULIAJI: Batshuayi, Benteke, Carrasco, E. Hazard, T. Hazard, R. Lukaku, Mertens, Mirallas, Origi








0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic