February 2, 2017

MBAO FC

Mbao FC si ya mchezo, kama ukibali waulize Mtibwa Sugar.

Mtibwa Sugar wamekutana na kipigo cha mabao 5-0 kutoka Mbao FC katika mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa CM Kirumba jijini Mwanza.

Mbao FC imepata mabao yake kufikia Yusuf Ndikumana aliyefunga mawili, mengine yakafungwa ni Steven Mugaya, Habibu Haji na Pius Charles.

Ushindi huo mkubwa kwa Mbao FC unakuwa ni tishio jingine kutokana na timu hiyo kushinda mfululizo.


Lakini Mtibwa Sugar iliyoonekana kuwa ngumu kutokana na uzoefu, ilionekana kuzidiwa kila idara.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic