November 11, 2016



Kuelekea kwenye fainali za Kombe la Dunia 2018, Brazil imeifunga Argentina mabao 3-0 katika mchezo uliochezwa alfajiri ya kuamkia leo Ijumaa.

Brazil ambayo ilipoteza makali katika miaka ya hivi karibuni, imepata ushindi huo kupitia kwa mabao ya Philippe Coutinho, Neymar na Paulinho.

Argentina ikiongozwa na nahodha wake, Lionel Messi ilishindwa kufurukuta licha ya kuchezeha kikosi kamili, hivyo imejiweka katika mazungira magumu ya kusonga mbele katika ukanda wa Amerika Kusini.















 Kwa sasa Argentina inashika nafasi ya sita kati ya 10 zinazowania nafasi ya kusonga mbele katika kusaka tiketi ya kucheza michuano hiyo mikubwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic