November 11, 2016

Wachezaji wakipiga selfie mbele ya jengo la ikulu.
Staa wa kikapu nchini Marekani katika Ligi ya NBA, LeBron James ameiongoza timu yake ya Cleveland Cavaliers kutembelea ikulu ya nchi hiyo kutokana na kutwaa ubingwa NBA msimu uliopita.

Wakiwa ikulu jana Alhamisi wachezaji wa timu hiyo walijumuika na rais wa nchi hiyo, Barrack Obama na mkewe, Michelle Obama ikiwa pia ni sehemu ya kumuaga kabla hajaondoka madarakani kumpisha Donald Trump ambaye amechaguliwa katika uchaguzi wa rais ulifanyika wiki hii.
 

Obama akikabidhiwa jezi ya Cleveland.







LeBron James akipiga selfie na mke wa Obama.



Michelle Obama akitaniana na wachezaji wa Cleveland.


James alikuwa ni sapota wa Hillary Clinton katikauchaguzi wa rais, lakini Donald Trump ndiye aliyeibuka mshindi.

Imekuwa ni kawaida timu inaposhinda NBA kupata nafasi ya kwenda kutembelea mjengoni hapo maarufu kwa jina White House.

Katika hotuba yake aliyoitoa kwa wachezaji hao, Obama alimsifia James kwa kuonyesha uwezo wa juu na kueleza kuwa ni mchezaji ambaye hana ubinafsi anapenda mafanikio ya wengi, anajituma na ana nidhamu ya kazi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic