November 22, 2016



Wakati mkataba wa nyota Lionel Messi unatarajia kufikia mwisho mwaka 2018, kuna klabu ambayo imetoa ofa ya day la usajili la euro million 100 litamlipa mshambuliaji huyo.

Sharti ambalo klabu hiyo imetoa ni Messi kutosaini mkataba mpya na Barcelona na badala yake imeweka mezani fedha hizo ambazo itamlipa Messi.

Gazeti la El Mundo la Hispania ndiyo limeandika habari hiyo lakini halijaeleza klabu hiyo ni ipi.

Tayari kulikuwa na taarifa kwamba Barcelona inataka kumuongezea Messi mkataba mpya, lakini inaonekana klabu nyingine zinataka Messi aondoke Barcelona nazo zip ate huduma yake.



Hata hivyo kwa wachunguzi wa mambo, inaonekana ni vigumu sana kwa Messi kuondoka Barcelona kwa kuwa maisha yake yamekuwa ndani ya klabu hiyo tokea akiwa na miaka 13 alipotoka kwao Argentika akiongozana na baba yake mzazi, Jorge Messi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic