December 24, 2016


Baada ya vinara wa Ligi Kuu Bara Simba kushindwa kumalizana na kiungo wake, Jonas Mkude juu ya kumwongezea mkataba mpya, nyota huyo amezua balaa jipya klabuni hapo ambapo ameugawa uongozi.

Viongozi wa Simba wanadaiwa kugawanyika makundi mawili juu ya mchezaji huyo ambapo baadhi yao wanataka aachwe baada ya mkataba wake kuisha lakini wengine wanataka aongezwe mkataba mpya.

Habari za kuaminika katoka ndani ya Simba zimedai kuwa viongozi wanaotaka Mkude aondoke ni wale ambao wanaamini kiungo James Kotei kutoka Ghana anaweza kuziba pengo la Mkude.

“Wale wanaotaka Mkude abaki wanaona kuwa Kotei hana uwezo wa kumshinda Mkude, hivyo endapo watamuacha aondoke basi pengo lake litawachukua muda mrefu kuliziba.

“Hali hiyo imefanya mpaka sasa Mkude kutopewa mkataba mpya licha ya matatizo yote yaliyojitokeza hapo awali kati yake na uongozi kuwa tayari yameshapatiwa ufumbuzi,” kilisema chanzo hicho cha habari.

Alipoulizwa Mkude kuhusu mkataba mpya, alisema: “Sijasaini na mpaka sasa sijui chochote kinachoendelea lakini hilo haliniumizi kichwa kwani mimi nafanya kazi yangu uwanjani.

“Inawezekana kuna mambo hayajakamilika lakini mimi sina tatizo watakaponiletea mkataba nitausaini kama utakidhi yale yote ambayo tulikubaliana.”

Alipotafutwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe hakupatikana, Katibu Mkuu wa Simba, Patrick Kahemele hakupokea simu lakini Makamu wa Rais wa klabu hiyo, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ alisema: “Sielewi lolote kuhusu suala hilo."

SOURCE: CHAMPIONI


2 COMMENTS:

  1. acha habar za uchonganishi una uhakika viongozi wamegawanyika? mbona uandik habar za club yako mechi ya jana walivyopigana umeishia kutoa tu matokeo ya live scores?

    ReplyDelete
  2. Kotei bado hajanishawishi ingawa pia muda una kauli zake

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic