December 17, 2016



Beki wa zamani wa Manchester United, Rio Ferdinand amerejea kwenye makao makuu ya klabu yake hiyo na kutembelea kwenye idara tofauti ukiwemo Uwanja wa mazoezi wa Carrington.
Rio na Pogba



Akiwa kwenye ziara hiyo ambayo ameweka video yake katika You Tube, Rio alipata nafasi ya kuonana na mastaa kadhaa wa timu hiyo pamoja na wachezaji vijana chini ya umri wa miaka 15 ambao walikuwa wametoka kufungwa mabao 9-0 na wapinzani wao wakubwa, Man City.


Ferdinand ambaye ana umri wa miaka 38 alionana na mchezaji aliyesajiliwa kwa bei kubwa zaidi duniani, Paul Pogba pamoja na Ashley Young naJesse Lingard.


Katika video hiyo, Rio anaonekana akipata mapokezi mazuri kila anapoingia huku Pogba akionekana kufurahi na kuanza kudansi akimfurahia mkongwe huyo.



Rio na mwalimu wa yoga.

Akiwapa ushauri Man United U15.

Rio akiingia jikoni kuwasapraizi wapishi.

Rio akiwa na Young na lingaad.

Enzi zake alipokuwa Man United.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic