Misri imetwanga Ghana kwa bao la Mohammed Salah aliyefunga katika dakika ya 11.
Ushindi wa bao 1-0 wa Misri unaifanya imalize ikiwa kinara wa Kundi D baada ya kufikisha pointi 7, inafuatiwa na Ghana yenye pointi 6 huku Mali yenye 2 na Uganda yenye moja ambazo leo zimetoka sare ya 1-1 zinarejea nyumbani.
Sasa Misri kama vinara wa Kundi D watakutana na Morocco huku Ghana wakikutana na DR Congo katika mechi za hatua ya robo fainali.
0 COMMENTS:
Post a Comment