January 25, 2017

Meneja wa Simba Mussa Hassan Mgosi alilazimika kufanya kazi ya ziada kuwajibu na kutuliza mzuka wa mashabiki wa Simba.

Mashabiki hao walimfuata Mgosi akiwa ametulia pembeni ya uwanja akifuatilia mazoezi ya Simba kwenye Uwanja wa Boko Veterani, jana jioni.

Mashabiki wa Simba walikuwa na kero kadhaa lakini suala la wafungaji ndio lilikuwa likiwakera zaidi.

Wengine waliamini wachezaji hawajalipwa mishahara yao kwa miezi kadhaa, jambo linalochangia wasicheze kwa kujituma.

Baada ya mashabiki kadhaa kuweka hewani malalamiko yao, Mgosi alimjibu mmoja baada ya mwingine kwa ufafanuzi mzuri na mwisho kukata kiu Yao.

Baadhi ya aliyowaeleza ni wao viongozi kuendelea kuwakumbusha wachezaji wao mara kwa mara kwamba Simba wanataka nini.

Lakini akawasisitiza mashabiki kuendelea kuwaunga mkono bila ya kujali wako katika wakati upi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic