February 21, 2017




Wachezaji 21 walio katika kikosi cha Simba kambini mjini Zanzibar, wako vizuri.

Taarifa za uhakika kutoka ndani ya kambi ya Simba mjini Zanzibar, wako katika hali nzuri pamoja na mazoezi mfululizo.

Simba ina wachezaji 21 walio kambini na wanaonekana kuwa tayari kwa ajili ya mechi ya Jumamosi dhidi ya Yanga ambao wameweka kambi Kigamboni mjini Dar es Salaam.

"Kweli wachezaji wote 21 wako vizuri kabisa na wanaendelea na mazoezi vizuri kabisa. Hivyo uamini hakuna majeruhi.

"Ilikuwa pekee Mwanjale ambaye lipewa mapumziko ya siku kumi. Lakini sasa amemaliza na amerejea tena mazoezini na kuungana na wenzake," kilieleza chanzo kutoka ndani ya Simba.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic