April 12, 2017



Nahodha wa Manchester United, Wayne Rooney ataondoka katika klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu.

Mmoja wa wachezaji wa timu hiyo ndiye aliyevujisha siri, kwamba Rooney hana raha na anaona ni wakati mwafaka kwake kuondoka Old Trafford kwa kuwa hapati nafasi ya kucheza.

Kocha Jose Mourinho anaonyesha kutomuweka Rooney kama chaguo la kwanza lakini mara kadhaa, naye amekuwa akiumia.

Rooney ambaye amecheza Man United kwa miaka 13 tokea alipojiunga nayo akiwa kinda kutoka Everton, amekuwa akiandamwa na mamumivu ambayo pia yamechangia akose mechi kadhaa.

Imeelezwa, hana uhakika pia kucheza mechi ijayo ya Man United ambayo itakuwa ya Europa League dhidi ya Anderlecht na itapigwa nchini Ubelgiji, Ahamisi.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic