Beki Marc Bartra ameifungia timu yake ya Borussia Dortmund moja ya mabao matatu wakati ikiilaza Wolfsburg 3-0.
Bartra ambaye ni Mhispania aliyetokea Barcelona, alionyesha hisia zake kwa kubusu kitambaa cheusi kwa ajili ya maombolezo yanayotokana na shambulizi la kigaidi jijini Barcelona, juzi.
Kisoka, beki huyo amekulia katika chuo cha watoto cha Barcelona, maarufu kama La Masia.
Mabao mengi ya Dortmund dhidi ya Wolfsburg yalifungwa na Christian Pulisic na Pierre-Emerick Aubameyang.
0 COMMENTS:
Post a Comment