February 16, 2018



Azam FC imeshindwa kuonyesha cheche katika Ligi Kuu Bara baada ya kutoka sare ya bila kufungana dhidi ya Lipuli ya Iringa.

Mechi hiyo kwenye Uwanja wa Samora mjini Iringa ilikuwa ni vuta nikuvute na hadi mwisho hakukuwa na mshindi.

Kwa sare hiyo, Azam FC imebaki na pointi 35 baada ya kucheza 19.

Hiyo inawafanya waendelee kubaki katika nafasi ya nne, huku wakizidiwa pointi mbili na Yanga walio katika nafasi ya pili.

Yanga iko katika nafasi ya pili ikiwa na pointi 37 na Simba ndiyo vinara wakiwa na 42.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic