Emmanuel Okwi ameipatia Simba bao la mapema kabisa katika kipindi cha pili, dakika ya 55.
Okwi amefunga bao hilo na kuifanya Simba kuwa mbele kwa bao 1-0. Mechi hiyo ni ya Kombe la Shirikisho.
HALF TIMA:
Mechi kati ya Gendamarie dhidi ya Simba sasa ni mapumziko.
Mechi hiyo imekuwa na ushindani mkubwa na Simba wamepoteza nafasi za tatu za kufunga za wazi huku wenyeji Gendamarie wakipoteza moja.
Simba wameonekana kushambulia lakini Gendamarie wako makini nao wamekuwa wakijibu mashambulizi tofauti na mechi ya kwanza ambayo walifungwa kwa mabao 4-0 mjini Dar es Salaam.








0 COMMENTS:
Post a Comment