April 26, 2018



Kiungo wa klabu ya Simba, Jonas Gerrard Mkude, amesema kuwa wanaendelez vema na maandalizi ya mchezo dhidi ya Yanga utakaopigwa Aprili 29 2018 katika Uwanja wa Taifa.

Simba itakuwa mwenyeji katika mpambano huo ulio na shauku kubwa kutoka kwa mashabiki na wadau wa soka la Tanzania.

Mkude ameeleza kuwa Simba wanahitaji kupambana ili kupata alama tatu muhimu zitazowafanya wazidi kutengeneza mazingira ya kuutwaa ubingwa wa ligi msimu huu.

“Mechi yetu na Yanga ni ngumu kwa sababu kila mmoja anajua ukubwa wa mchezo wenyewe ambao mara nyingi huwa na ush­indani.

“Kikubwa tunachotak­iwa kukifanya ni kupata sapoti na ushirikiano baina ya wachezaji katika mchezo huu ambapo uwezo wa timu kwa jumla ndiyo utaka­oamua ushindi,” alisema Mkude.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic