May 8, 2018


Leicester inamtaka meneja wa Hudderfield David Wagner kuwa mkufunzi wao mpya , Foxes wanatarajia kumuaga meneja wao Claude Puel mwezi huu. (Times - subscription required)

Mshambuliaji wa Chelsea na Ubelgiji Eden Hazard ,27, amesema ''hana nafasi'' ya kuondoka Stamford Bridge kuelekea Manchester United. (Mail)

Mshambuliaji wa Chelsea na Uhispania Alvaro Morata , 25, ana uwezekano wa kurudi Juventus na Chelsea wanaweza kufikiria uhamisho wa mshambuliaji wa Paris St-Germain na Uruguay Edinson Cavani , 31. (Tuttosport, via Metro)

Arsenal inamtaka meneja wa Juventus Massimiliano Allegri au kocha wa zamani wa Barcelona Luis Enrique kuwa mkufunzi wao mpya, lakini wawili hao bado wanawasiwasi kuhusiana na uongozi wa klabu hiyo. (Sky Sports)

Enrique yuko katika hali ya kutaka kiwango kikubwa cha malipo yake iwapo atakuwa meneja mpya wa Arsenal- baada ya kutaka kulipwa £15m baada ya kukatwa ushuru. (Mirror)

Meneja wa Napoli Maurizio Sarri ambaye amehusishwa na Chelsea ametoa pendekezo la kuiaga upande wa klabu hiyo ya Serie A wakati wa majira ya joto iwapo atadhibitisha kuna kifungu cha kutolewa kwa yuro milioni 8 katika mkataba wake. (Talksport)

Liverpool imezungumza na Juventus kuhusu mkataba wa Sami Khedira mwenye umri wa miaka 31 wakati wa uhamisho wa bure kwa kiungo wenzake Mjerumani Emre Can, 24, kuelekea upande wa Italia. (Sun)

Bayern Munich wako tayari kumuuza mshambuliaji raia wa Poland Robert Lewandowski, 29, anayetegewa na Manchester United. (Calciomercato, via Express)

Kutoka BBC

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic