May 2, 2018



Tukio la mchezaji wa Yanga, Kelvin Yondani limezidi kuzungumziwa na wadau mbalimbali wa soka kwa namna yake kutokana na kitendo cha kumtemea mate beki wa Simba, Asante Kwasi katika mechi ya ligi dhidi ya Simba iliyopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa zamani wa Simba, Hassan Dalali, naye amefunguka kwa kueleza kuwa hajafurahishwa na kitendo hicho alichofanya Yondani kwa kinashusha heshima yake ndani ya soka la Tanzania.

Kupitia Spoti Leo ya Radio One, Dalali ambaye aliwahi kuingoza Simba kwa mafanikio, amesema Yondani alikosea na si vema tukio kama hilo likajirudia kwani halipendezi hata kidogo.

"Kwakweli si kitendo kizuri, Yondani alikosea na si vema mambo kama haya yakifanyika kwa wachezaji wetu kwa maana hayapendezi hata kidogo" alisema Dalali.

1 COMMENTS:

  1. Mimi inanistaajabisha kuwa hawezi kuchukuliwa hatua Simba ipeleke mashitaka na hapa inaonesha huu ni muelekeo mpya wa ajabu na kuchekesha.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic