BAADA YA KUITWANGA BRAZIL 2-1, UBELGIJI IMETENGENEZA REKODI HIZI BAB-KUBWA
Baada ya kuitwanga Brazil kwa mabao 2-1, Ubelgiji imefanikiwa kuingia nusu fainali ikiwa ni mara ya pili kwao kufika hatua hiyo.
Mara ya kwanza na ya mwisho kufika hatua hiyo ilikuwa ni mwaka 1986 katika michuano iliyofanyika nchini Mexico.
Katika robo fainali, Ubelgiji waliifunga Hispania kwa penalti 5-4 baada ya sare ya 1-1 katika dakika 120.
Katika nusu fainali, safari yao ilisitishwa na Argentina baada ya kuwafunga mabao 2-0.
Katika Kombe la Dunia huko Mexico, Argentina ndiyo waliibuka mabingwa wakiifunga Ujerumani kwa mabao 3-2 katika fainali.
0 COMMENTS:
Post a Comment